MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA 2014/2015

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI


Simu:022-2110146/2110150/2/211679 Faksi:022-2113271, Tovuti: www.moe.go.tz

 NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA KWA MWAKA WA MASOMO 2014/2015



UTANGULIZI

Moja ya mikakati ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika kuandaa walimu mahiri ni pamoja na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya Stashahada ni wale wenye ufaulu mzuri katika mitihani ya kidato cha NNE na SITA. Ili kufanikisha azma hii, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, itadahili wanafunzi wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi Daraja la Tatu tu.

Aidha, kutokana na upungufu mkubwa wa walimu wa Sayansi na 
Hisabati wa takribani walimu 26,000 kipaumbele katika udahili kitatolewa kwa waombaji waliofaulu masomo Sayansi na Hisabati ili kuziba pengo hili. Nia ya Serikali ni kuwavutia wanafunzi wengi wa masomo ya Sayansi na Hisabati. Kuanzia mwaka huu wa masomo 2014/15 wanafunzi watakaojiunga na fani ya Ualimu kwa masomo ya Sayansi na Hisabati watagharimiwa na Serikali kupitia mfumo wa ruzuku na mkopo. Wanafunzi watakaokuwa na ufaulu wa Daraja la Kwanza watapatiwa Ruzuku na wale wenye Daraja la Pili na la Tatu watapewa mkopo ili kuwasaidia katika masomo yao. Watakaofaulu mafunzo ya ualimu katika masomo ya Sayansi/Hisabati watapatiwa ajira moja kwa moja kulingana na taratibu za serikali.

VIGEZO
Vigezo vifuatavyo vitatumika kuchagua wanachuo wa kujiunga na mafunzo ya ualimu mwaka 2014/15.

1:      MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA:  MASOMO YA SAYANSI/HISABATI NA UFUNDI:  MUDA MIAKA 2.

(i)         Ualimu wa masomo ya Sayansi/Hisabati katika vyuo vya Dakawa, Kasulu, Korogwe, Morogoro, Mpapwa, Tukuyu, Songea , Butimba, Kleruu na Monduli

Mwombaji awe amehitimu:
Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013 na awe na ufaulu wa ‘Principal Pass’ mbili  katika Masomo ya Sayansi na Hisabati.

(ii)        Ualimu wa ufundi katika chuo cha ualimu Kleruu
Mwombaji awe amehitimu:
a.   Mafunzo ya FTC kati ya mwaka 2004 na 2010 kutoka Vyuo vya Ufundi, Au
b.   Mafunzo ya ufundi katika ngazi ya NTA Level 6 au sifa linganishi (equivalent qualification) kati ya mwaka 2007 na 2013 kutoka chuo chochote cha Ufundi kinachotambulika na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).

(iii)       Ualimu wa Kilimo katika chuo cha ualimu Monduli
Mwombaji awe amehitimu:
Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013 na awe na  ufaulu ‘Principal Pass’ mbili katika somo la ‘Agricultural science’ na ‘Biology’, ‘Chemistry’ au ‘Food and Nutrition’.


2:         MAFUNZO MAALUM YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA KWA KIDATO CHA NNE MASOMO YA SAYANSI/HISABATI NA ENGLISH: MUDA  MIAKA 3

Ualimu wa masomo ya Sayansi/Hisabati na English katika vyuo vya Butimba, Morogoro, Korogwe, Songea na Mpwapwa

Mwombaji awe amehitimu:
Kidato cha IV kati ya mwaka 2004 na 2013 na awe na ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi la Tatu, na Credit mbili (yaani A, B+, B au C) katika masomo ya Sayansi, Hisabati na Kiingereza.

3:         MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA: MUDA MIAKA 2.
(i)         Ualimu wa masomo ya Sayansi Jamii katika vyuo vya Bunda, Dakawa Kasulu, Korogwe, Marangu, Morogoro, Mpwapwa, Mtwara (K), Shinyanga, Songea, Tabora, Tukuyu.

Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013 na awe na ufaulu wa kiwango cha  ‘Principal Pass’ mbili


(ii)        Biashara katika vyuo vya Shinyanga na Kasulu
Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013 na awe na ufaulu wa kiwango kisichopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja

(iii)       Sanaa za Ufundi, Sanaa za Maonyesho, Muziki na Michezo katika chuo cha Butimba.
Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013 na awe na ufaulu wa kiwango kisichopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja

Tanbihi: Masomo ya ‘Economics’, Basic Applied Mathematics’, ‘General Studies’ na ‘Divinity’ hayatatumika kama kigezo cha kumchagua au kumdahili mwombaji.

4:      MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI STASHAHADA ELIMU YA MSINGI: MUDA MIAKA 3)

Ualimu wa Stashahada ya  Elimu ya Msingi katika chuo cha Vikindu

Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha IV kati ya mwaka 2004 na 2013 wenye ufaulu wa Daraja la I Daraja la Tatu katika Mtihani uliofanyika katika kikao kimoja.

Tanbihi: Kipaumbele kitatolewa kwa waombaji waliofaulu masomo ya ‘Mathematics’, ‘Biology’, ‘Physics’, ‘Chemistry’,  ‘Agriculture’, ‘Food and Nutrition’, ‘English’ na Kiswahili na wahitimu wenye mahitaji maalumu.


5.      MAFUNZO YA UALIMU KAZINI STASHAHADA:- MUDA MIAKA 2

Ualimu wa masomo ya Sayansi katika vyuo vya Dakawa, Kasulu, Korogwe, Morogoro, Mpapwa, Tukuyu, Songea , Butimba, Kleruu na Monduli

Mwombaji awe amehitimu:
Mwalimu wa Daraja ‘A’ aliyehitimu Kidato cha VI na mwenye ufaulu usiopungua ‘Principal Pass’moja na ‘Subsidiary’ moja katika Masomo ya Sayansi na Hisabati; na mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili.


6:      MAFUNZO YA UALIMU KAZINI STASHAHADA (SEKONDARI):- MUDA MIAKA 2.

(i)         Ualimu wa masomo ya Sayansi Jamii katika vyuo vya Bunda, Dakawa, Kasulu, Korogwe, Marangu, Morogoro, Mpwapwa, Mtwara (K), Shinyanga, Songea, Tabora, Tukuyu.

Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013 na mwenye ufaulu usiopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja katika masomo ya ‘Biology, ‘Chemistry’ na ‘Food and Nutrition

(ii)        Ualimu wa masomo ya Biashara katika vyuo vya Shinyanga, Kasulu

Mwombaji awe:
Mwalimu wa Daraja ‘A’ aliyehitimu Kidato cha VI na mwenye ufaulu usiopungua ‘Principal Pass” moja na ‘Subsidiary’ moja; na mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili.

(iii)       Ualimu wa masomo ya Elimu Maalumu katika chuo cha Patandi
Mwombaji awe:

Mwalimu mwenye Stashahada ya Ualimu fani ya Sayansi; Au Sayansi ya Jamii na uzoefu wa kazi ya ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili, Au

Mwalimu wa Daraja ‘A’ aliyehitimu Kidato cha VI na mwenye ufaulu usiopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja; na mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili.

Tanbihi: Walimu wanaofundisha watoto wenye mahitaji maalum kama wasioona, viziwi, wenye ulemavu wa akili, n.k. ni sifa ya nyongeza (vithibitisho viambatishwe).


7:      MAFUNZO YA UALIMU KAZINI STASHAHADA ELIMU YA MSINGI:  MUDA MIAKA 2:

Ualimu wa Stashahada ya  Elimu ya Msingi katika chuo cha Vikindu
Mwombaji awe:
Mwalimu wa Daraja ‘A’ mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili.

MAELEZO MUHIMU
(i)            Vigezo vilivyoelekezwa kwa waombaji wa mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada ni kwa ajili ya waombaji wa mafunzo ya Ualimu katika Vyuo vya Ualimu vya Serikali na visivyo vya Serikali;
(ii)          Muombaji wa chuo cha ualimu cha Serikali anatatakiwa kuchagua vyuo visivyopungua vitano ambavyo angependa kujiunga navyo akianzia kile anachokipendelea zaidi;
(iii)         Waombaji wa mafunzo ya Ualimu walioajiriwa watakaopatiwa nafasi za mafunzo watapaswa kupata ruhusa (Release) kutoka kwa waajiri wao;
(iv)         Majibu kwa watakaochaguliwa kujiunga na mafunzo ya Ualimu katika vyuo vya Serikali yatatolewa kwenye Tovuti za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (www.moe.go.tz), OWM-TAMISEMI (www.pmoralg.go.tz) na NACTE (www.nacte.go.tz)
(v)           Waombaji watakaochaguliwa watatumiwa barua za kujiunga na mafunzo na Wakuu wa vyuo vya Ualimu watakakokuwa wamepangwa kupitia anuani zao;
(vi)         Tangazo hili lipo pia katika tovuti ya Wizara: www.moe.go.tz, OWM TAMISEMI: www.pmoralg.go.tz na NACTE: www.nacte.go.tz na kwenye ofisi za Makatibu Tawala (M) na vyuo vya ualimu;

Namna ya kutuma maombi:
a)    Waombaji watume maombi yao kwa njia ya MTANDAO(online application) kupitia tovuti zifuatazo: www.moe.go.tz  AU  www.nacte.go.tz
Maombi kwa njia ya mtandao yataambatana na ada ya shilingi 10,000 itakayolipwa kwa kutumia MPESA. Maelekezo ya kina kuhusu namna ya kutuma maombi kwa njia ya mtandao yanapatikana katika tuvuti ya wizara www.moe.go.tzna Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi www.nacte.go.tz

Malipo ya maombi yanaweza kufanyika kupitia MPESA kama ifuatavyo:
1.       Piga *150*00#
2.      Chagua 4. (Lipa kwa MPESA);
3.      Chagua 1. (Weka LIPA Namba);
4.      Weka LIPA Namba (ingiza namba 607070);
5.      Ingiza kiasi (ingiza kiasi cha 10,000.00);
6.      Weka Enter Reference No. ( ingiza 1234);
7.      Weka namba ya SIRI (ingiza namba yako ya siri); na
8.      Ingiza 1 kuthibibitisha malipo.
AU
b)    Barua kwa:
KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
S.L.P. 9121
DAR ES SALAAM (Aione: Mkurugenzi, Elimu ya Ualimu)
MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA 2014/2015 MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA  2014/2015 Reviewed by Unknown on 10:43:00 AM Rating: 5

JOBS CATEGORY

Tanzania Kenya NGO JOBS Uganda Best Jobs Consultancy Rwanda ICT JOBS Administrative United Nations Sudan Best Jobs Finance Health - Medical Engineering Ethiopia Education Agricultural Lecturer Human Resources Somalia Media Congo - Kinshasa Legal Jobs Bank Jobs Monitoring and Evaluation Mining World Vision Burundi Procurement African Barrick Gold Accountant Zambia Sales and Marketing US EMBASSY East African Community Mozambique Telecoms Research CARE International Save The Children Plan International Arusha Malawi South Sudan Oxfam Scholarships African Development Bank Finance and Administration SafariCom Aviation The Commonwealth American Embassy Sales Zanzibar Environmental Catholic Relief Services Dar es salaam USAID Operations FHI 360 UNDP Security World Bank Economist TradeMark East Africa Unicef Hospitality Managers International Rescue Committee (IRC) Restless Development Accounting Civil Engineers AMREF Morogoro Utumishi AfDB African Development Bank COOPI - Cooperazione Internazionale Driver - Logistics Path International Mwanza African Union Tigo Jobs Marketing Mbeya Teaching Au African Union PSI Population Services International Pwc PricewaterhouseCoopers East African Breweries North Mara Gold Mine ACTED Djibouti Malaria Consortium Bulyanhulu Gold Mine DFID Driver Buzwagi Gold Mine Jhpiego COMESA FINCA JOBS International Jobs Adeso Danish Refugee Council Kilimanjaro Nairobi Coca-Cola Handicap International Pact International Rio Tinto Solidarités International Tender EGPAF Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation Logistics Serengeti Breweries Ltd Nation Media Group Africare Norwegian Refugee Council Samaritan's Purse Chemonics International COUNTRY DIRECTOR ICAP of Columbia University InterShips Precision Air RwandAir Marie Stopes International (MSI) Serengeti Breweries Volunteer Climate Change IGAD Tetra Tech ARD Agriculture Jobs Dodoma Iringa One Acre Fund Project Management Clinton Health Access Initiative (CHAI Technoserve Twaweza East Africa ActionAid Lutheran World Federation SADC Secretariat Tanga Vso International ACDI/VOCA Halmashauri Agha Khan Kenya Commercial Bank World Agroforestry Centre Deloitte East Africa International Organization for Migration (IOM) COMESA Secretariat: Software Engineering Safety and Security Shinyanga Jobs Tanzania Breweries Pathfinder International World Health Organization KPMG TANROADS Tanzania Electric Supply Company British Council Futures Group KCB BANK UN-Habitat WFP World Food Programme Barclays GEITA GOLD MINING TANESCO Electrical Engineer Food and Agriculture Organization GOAL Mombasa Tabora WWF World Wide Fund for Nature Microsoft Tanzania Ports Authority East African Development Bank Family Health International (FHI) IBM EAST AFRICA IntraHealth International Mercy Corps SERIKALINI - GOVERNMENT OF TANZANIA AccessBank Community Development Jobs Data Base Management Google Africa ICAP - TZ KEMRI/CDC Program WaterAid Tanzania Auditor SNV International Stanbic Bank Amnesty Horn Relief Kampala Management Systems International (MSI) Standard Chartered Bank VETA Christian Aid DIAMOND TRUST BANK Helen Keller International Help Age Mtwara Uganda Telecom Airtel Africa Equity Bank Internships Marie Stopes TCRA Web Development B B C WORLD SERVICE Human Rights Kigali Makerere University Nile Basin Initiative Kenyatta University Kigoma Mzumbe University NSSF National Social Security Fund Nile Breweries Limited Tulawaka Gold Mine University of Nairobi kenya Airways Bank of Tanzania Graduates MTN Muhimbili National Hospital Nepad Partners in Health Room to Read SUMATRA UNWOMEN African Wildlife foundation (AWF) KEMRI Kagera Librarian MENTOR Initiative Trainee USAILI - INTERVIEW Uiversity of Nairobi WaterAid International icipe Project CAFOD - Catholic Agency for Overseas Development Egerton University EngenderHealth Goal Ireland Kenyan Banks Lake Victoria Basin Commission Peace Corps TANAPA TASAF Tanzania Social Action Fund Zanzibar University ACB AKIBA COMMERCIAL BANK AGRA Alliance for a Green Revolution in Africa Advans Bank Ethiopian Airlines Freedom House IITA International Institute of Tropical Agriculture Legal Moshi NMB BANK Resolute Tanzania Singida Uganda Uganda National Roads Authority University of Dar es salaam University of Dodoma British High Commission ChildFund EWURA FilmAid International NECTA TPDC Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) United States International University World Concern Aga Khan Foundation CBA Commercial Bank of Africa Ecomist Ernst and Young IUCN International Union for Conservation of Nature International Medical Corps Islamic Relief Kakira Sugar Musoma National Institute for Medical Research OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA Relief International TAA Tanzania Airports Authority Trócaire Uganda Revenue Authority VODACOM TANZANIA VSF Belgium Architects Hivos IFC International Finance Corporation Ifakara Health Institute Inoorero University International Commercial Bank Kenya Red Cross Society MADEREVA Medical Oil and Gas Pwani University College SOKOINE UNIVERSITY Tumaini University Water Engineering AWF African Wildlife Foundation Acacia Mining Accounts African Virtual University Altima Africa Ardhi University Bank of Uganda Business Development Concultancy Del Monte Kenya Embassies Kenya Airports Authority Lake Victoria South Water Services Board Mara National Bank of Commerce RECORDS MANAGEMENT JOBS RUKWA Ruvuma Search for Common Ground Songea TTCL Tanzania Telecommunications Company Limited Unilever War Child International Zinduka Afrika ACORD AKU ​Aga Khan University Africa Nazarene University Africa Rice Center (AfricaRice) Aga Khan Health Services CRDB BANK Commercial Bank of Africa Daraja Tanzania Engineers Registration Board (ERB) Fina Bank International Potato Center International Potato Center (CIP) Intrahealth Jomo Kenyatta University Kilimanjaro Christian Medical Centre Kyambogo University Lindi Jobs MCL Mwananchi Communications MUHAS-harvad Moi University NBC BANK National University of Rwanda Ngorongoro Conservation Area Authority Njombe Nuru International Nzoia sugar Company RTI International SUA SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE THE LAW SCHOOL OF TANZANIA TRA Tanzania Revenue Authority Tanzania Postal Bank The Foundation For Civil Society Udhamini wa Masomo Western Union AIR TANZANIA Action Against Hunger (ACF) Agricultural Society of Kenya BRALIRWA Bondo University College Caritas Comoros Concern Worldwide Conservation Jobs Consolidated Bank of Kenya DHL Express Ewaso Ngiro South River Basin Development Authority Geologist Gulf African Bank INSTITUTE OF ADULT EDUCATION Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology Kabale University Kabale University (KAB) Kenya Ports Authority KickStart International MORUWASA Morogoro Urban Water and Sanitation Authority MSH Management Sciences for Health Mumias Sugar Company Nairobi Hospital Nkumba University Rural Electrification Agency SOKINE UNIVERSITY SONGWE STAMIGOLD Stores TACAIDS TARURA TCU Tanzania Commission for Universities Tullow Oil World Lung Foundation (WLF) ALAF Limited Aga Khan Development Network (AKDN) Aga Khan Hospital Air Malawi American Refuge Committee BENKI YA POSTA - TPB BANK BTC Belgian Technical Cooperation Bhttp://www.blogger.com/img/blank.gifank of Tanzania Bioversity International CHF International Customer Service Jobs DANGOTE DIT DAR ES SALAAM INSTITUTE OF TECHNOLOGY Danida Dar es Salaam Institute of Technology Daystar University ECOBANK ETDCO Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Company European Union IFM INSTITUTE OF FINANCE MANAGEMENT INSURANCE JOBS - BIMA ITECH Internews® Network KUITWA KAZINI Kenya Accreditation Service Kenya Polytechnic University College Kilombero Sugar Company Kisii University College Kisumu Laboratory Jobs MSD MEDICAL STORES DEPARTMENT MSF Switzerland Management Sciences for Health Manyara Maseno University Ministry of State for Planning Muteesa 1 Royal University Médecins Sans Frontières NIDA National Identification Authority Narok University College OSHA Occupational safety and Health Authority Open Society Initiative for Eastern Africa (OSIEA) PA PAC PEPSI POLICE - POLISI Petroleum EngineerS RWANDA HOUSING AUTHORITY Seychelles Songas TBC TANZANIA BROADCASTING CORPORATION TBS TANZANIA BUREAU OF STANDARDS TFDA TANZANIA FOOD AND DRUGS AUTHORITY TIB - Tanzania Investment Bank Tanzania Mortagage Refinance Company Tanzania Teachers’ Union Transmara Sugar Company Tropical Pesticides Research Institute Tumba College of Technology Twiga Cement UNESCO UNOCHA Umma University University WRP Walter Reed Project ZANTEL ao uga
Powered by Blogger.