TANGAZO LA KAZI UTUMISHI - KISWAHILI - 23 Januari, 2015

Kumb. Na EA.7/96/01/H/34                                                           23 Januari, 2015


Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni chombo ambacho kimeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu 29(1). Kwa mujibu wa Sheria hiyo, chombo hiki, pamoja na kazi zingine kimepewa jukumu la kutangaza nafasi wazi za kazi zinazotokea katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Waajiri (Taasisi za Umma).

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi kwa

Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 121 za kazi kwa ajili ya Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala wa serikali na Mamlaka za serikali za mitaa

1.0           AFISA MISITU DARAJA LA II (FOREST OFFICER GRADE II) – NAFAS 5

1.1   MAJUKUMU YA KAZI
·         Kusimamia upandaji na uhudumiaji wa miti na misitu.

·         Kusimamia uendelezaji wa misitu ya kupandwa isiyozidi hekta 5,000 au ya asili isiyozidi hekta 10,000.

·         Kufanya utafiti wa misitu.

·         Kutekeleza Sera na Sheria za misitu.

·         Kuendesha mafunzo ya Wasaidizi Misitu.

·         Kukusanya takwimu za misitu.

·         Kufanya ukaguzi wa misitu.

·         Kupanga na kupima madaraja ya mbao.

·         Kudhibiti leseni na uvunaji wa miti.

·         Kutoa ushauri na mafunzo kwa wananchi juu ya uendelezaji na matumizi endelevu

ya miti na  kwa wananchi.

·         Kufanya ukadiriaji wa rasilimali za misitu.

·         Kupima maeneo na kuchora ramani za misitu.

1.2   SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye Shahada ya Misitu kutoka chuo Kikuu cha kilimo cha Sokoine au Vyuo Vikuu vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

1.3   MSHAHARA

·         Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.D kwa mwezi.

2.0           MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA III – NAFASI 7

2.1   MAJUKUMU YA KAZI
·         Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi

·         Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi

·         Kusimamia shughuli za uwindaji wa kitalii na utalii wa picha

·         Kulinda binadamu na mali zake dhidi ya Wanyamapori

·         Kukusanya na kulinda Nyara za Serikali

·         Kufanya usafi na ulinzi wa kambi

·         Kusimamia uingiaji na utokaji wa watu na mali zao kwenye hifadhi

·         Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani

·         Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na kukusanya takwimu zao

·         Kusimamia taratibu za kusafirisha wanyamapori hai na nyara nje na ndani ya Nchi

·         Kudhibiti wanyamapori waharibifu

·         Kudhibiti moto kwenye hifadhi

·         Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake

2.2   SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Astashahada au Astashahada ya awali ya Uhifadhi wa Wanyamapori (Technician or Basic Technician Certificate in Wildlife Management) kutoka Chuo cha Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi au chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

2.3   MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B1 kwa mwezi

3.1         AFISA MTENDAJI WA KATA DARAJA LA III (WARD EXECUTIVE OFFICER

GRADE III) – NAFASI 30

3.1   MAJUKUMU YA KAZI

·         Atakuwa Mtendaji Mkuu wa Kata na kiungo cha Uongozi kwa Idara zote katika kata na atashughulikia masuala yote ya kata

·         Atakuwa Mhamasishaji mkuu wa Umma katika mikakati mbalimbali ya uzalishaji, mali, kuondoa njaa na Umasikini.

·         Atakuwa ni Katibu wa kamati ya maendeleo ya kata.

·         Ataratibu na kusimamia upangaji wa shughuli za maendeleo ya kata, vijiji na vitongoji.

·         Atatafsiri sera na kusimamia utekelezaji wa sheria ndogondogo katika Kata yake.Atamsaidia Mkurugenzi Kuratibuna kusimamia shughuli za Uchaguzi katika Kata.



·         Kumsaidia na kumwakilisha Mkurugenzi katika kusimamia maendeleo ya eneo lake.

·         Kusimamia utendaji kazi wa wataalamu na watendaji wengine katika ngazi ya Kata.

·         Kuratibu na kuandaa taarifa za utekelezaji na kuziwasilisha kwa mkurugenzi na nakala kwa Katibu Tarafa.

·         Atakuwa mwenyekiti katika vikao vya vinavyowahusisha wataalamu na watendaji wa vjiji, na NGO’S katika kata yake.

·         Atakuwa Msimamizi na mratibu wa takwimu zote zinazokusanywa katika vijiji, vitongoji, na kata yake.

3.2   SIFA ZA MWOMBAJI.

·         Kuajiriwa waliohitimu kidato cha nne au sita na mwenye cheti cha Mafunzo ya Stashahada katika fani ya Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii (Sociology), Maendeleo ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Uchumi na Mipango kutoka chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo Dodoma au chuo chochote kinachotambulika na Serikali.

3.3   MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia viwango vya Serikali ngazi ya Mshahara TGS C kwa mwezi.

4.1         AFISA KILIMO DARAJA LA II (AGRO – OFFICERS) – NAFASI 10

4.1   MAJUKUMU YA KAZI
·         Kuthibiti visumbufu vya mazao na mimea,

·         Kukusanya takwimu za bei za mazao kila wiki na kila mwezi,

·         Kukusanya takwimu za upatikanaji wa mazao katika masoko kila wiki/kila mwezi,

·         Kuendesha mafunzo ya wataalam  wa kilimo,

·         Kufanya ukaguzi wa ubora na matumizi ya pembejeo na zana,

·         Ufuatiliaji wa mwenendo wa soko la mazao ya biashara,

·         Kuendesha mafunzo juu ya hifadhi bora ya udongo na maji,

·         Kutoa habari juu ya teknolojia mpya kwa wadau,

·         Kuandaa/kuandika taarifa za utekelezaji kwa sekta ndogo ya mazao,

·         Kusimamia/kuendeleza taaluma ya uzalishaji mboga, matunda, maua na mazao mengine,

·         Kusimamia/kuendeleza uzalishaji wa mbegu bora,

·         Kuandaa, kutayarisha kufunga na kusambaza mbegu bora,

·         Kufanya majaribio ya magonjwa kwenye mbegu,

·         Kufanya ukaguzi wa mbegu mpya kwa kushirikiana na watafiti wa mbegu kabla ya kupitishwa,

·         Kuendesha mafunzo ya kuzalisha mboga, matunda, maua na viungo,

·         Kuhamasisha uzalishaji wa mazao ya bustani,

·         Kufanya utafiti mdogo mdogo wa mazao yanayofaa kulimwa katika sehemu ya kilimo cha umwagiliaji,

·         Kufanya utafiti wa udongo,

·         Kuhamasisha uanzishaji wa vikundi vya wakulima/wamwagiliaji,


·         Kuzalisha mbegu za msingi baada ya kuzalishwa na watafiti,

·         Kuendesha/kusimamaia vishamba vya majaribio vya mbegu na uchunguzi maabara ili kuondoa utata juu ya mbegu.

4.2   SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza (bachelor degree) ya kilimo au shahada ya sayansi waliojiimarisha katika mchepuo wa kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

4.3   MSHAHARA

·         Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS D Kwa mwezi.

5.1         AFISA KILIMO MSAIDIZI DARAJA LA II (AGRICULTURAL FIELD OFFICERS)

– NAFASI 12

5.1   MAJUKUMU YA KAZI
·         Kushirikiana na watafiti kuendesha vishamba vya majaribio,

·         Kukusanya/kuhifadhi takwimu za majaribio,

·         Kuwafundisha wakulima mbinu za kilimo bora,

·         Kuwafikishia wakulima matokeo ya utafiti,

·         Kuwafundisha wakulima mbinu bora za kilimo, matumizi ya mbolea na madawa, pembejeo za kilimo,

·         Kukusanya na kutunza takwimu za mazao na bei kwa wiki mwezi, robo na mwaka ngazi ya halmashauri,

·         Kukusanya takwimu za mvua,

·         Kushiriki katika savei za kilimo,

·         Kushirikiana na vikundi vya wakulima kuhusu matatizo na teknolojia sahihi za kutumia,

·         Kupanga mipango ya uzalishaji,

·         Kupima uotaji wa mbegu na kusimamia taratibu za ukaguzi,

·         Kutathmini na kusavei maeneo ya vyanzo vya maji kwa ajili ya kuhifadhi,

·         Kutunza miti mizazi,

·         Kuwatambua wasambazaji wa pembejeo,

·         Kutoa mafunzo ya lishe kwa wakulima,

·         Kufanya vipimo vya ubora, unyevunyevu na uotaji wa mbegu,

·         Kusimamia taratibu za ukaguzi,

·         Kudhibiti visumbufu vya mazao na mimea,

·         Kusimamia shughuli za kila siku za majaribio ya kilimo,

·         Kuwaelimisha wakulima juu ya matumizi bora ya udongo na maji,

·         Kutoa ushauri wa kilimo mseto,

·         Kuandaa sheria ndogo za hifadhi ya mazingira na

·         Kutoa taaluma ya uzalishaji wa mboga, matunda, maua na viungo.


5.2    SIFA ZA MWOMBAJI



·         Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha nne au Sita (VI) wenye stashahada (Diploma) ya kilimo kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

5.3   MSHAHARA

·         Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS C Kwa mwezi.

6.1         MTAKWIMU DARAJA LA II (STATISTICIAN GRADE II) – NAFASI 5

6.1   MAJUKUMU YA KAZI
·         Kubuni na kuendeleza mfumo wa kitaifa wa kukusanya  na kuratibu takwimu

·         Kutengeneza utaratibu wa kukusanya takwimu pamoja na ule wa kuchukua takwimu za mfano/vielelezo (Sampling)

·         Kukusanya, Kuchambua na kuwasilisha takwimu ngazi za juu.


6.2   SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza katika fani ya Takwimu au Hisabati au sifa zinazolingana na hizo kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali na wenye ujuzi wa kutumia Kompyuta.

6.3   MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwe

7.1         AFISA UGAVI MKUU DARAJA LA I - NAFASI 1(INARUDIWA)

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Afisa Mtendaji Mkuu Wakala wa Vipimo (WMA)

7.1   MAJUKUMU YA KAZI
·         Kushauri juu ya Sera ya Ununuzi na Ugavi katika Wakala;

·         Kushauri juu ya Mfumo wa Mtandao wa Ununuzi na Ugavi kwa kutumia kompyuta,

“e-procurement”;

·         Kutathmini taarifa ya vifaa vinavyotumika na Wakala ili kujua aina ya kasi ya vifaa husika kwa hatua zaidi;

·         Kusimamia utayarishaji wa Mpango wa manunuzi wa Wakala;

·         Kusimamia utayarishaji wa makisio ya vifaa vinavyohitajika katika Wakala;

·         Kusimamia upimaji wa utendaji wa Maafisa Ugavi walio chini yake;

·         Kumshauri Mtendaji Mkuu kuhusu namna bora kutekeleza majukumu yanayohusu ununuzi, utunzaji na ugavi katika Wakala;


7.2   SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye Shahada ya Ugavi na Shahada/Stashahada ya Uzamili katika fani za Biashara au Ugavi kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Bodi ya Taifa ya Usimamizi wa Vifaa, na uzoefu wa kazi usiopungua miaka kumi na mbili (12).

7.3   MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani WMAS 7 kwa mwezi

8.0         AFISA VIPIMO DARAJA LA II- NAFASI 1 (INARUDIWA)

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Afisa Mtendaji Mkuu Wakala wa Vipimo (WMA)

1.1.2  MAJUKUMU YA KAZI

·         Kukagua, kuhakiki na kuvirekebisha vipimo vya wafanyabiashara;

·         Kutunza na kuhifadhi vifaa vya kitaalamu vitumikavyo katika utendaji wa kazi;

·         Kutoa ushauri kuhusu masuala ya uhakiki na matumizi ya vipimo;

·         Kufanya upelelezi kuhusu ukiukwaji wa Sheria ya vipimo;

·         Kupokea na kufanyia kazi malalamiko ya wadau na wateja;

1.1.3  SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa mwenye Shahada ya kwanza katika fani ya Legal Metrology au Legal and Industrial Metrology kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali. Au

·         Kuajiriwa mwenye Shahada katika fani ya Uhandisi / Sanyansi ambao wamepata crash programme in Legal and Industrial Metrology isiyopungua miezi mine (4) kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali. Au

·         Kuajiriwa mwenye Shahada katika fani ya Uhandisi / Sayansi ambao wamehitimu Stashahada ya Uzamili (Postgraduate Diploma) katika fani ya Vipimo kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali.

·         Kuajiriwa mwenye Stashahada ya juu katika fani ya Legal Metrology / Legal and Industrial Metrology kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali.

1.1.4  MSHAHARA

·         Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani WMAS3 kwa mwezi.


9.1         MHANDISI DARAJA LA II (MAJI) – WATER RESOURCE ENGINEER – NAFASI 6 (INARUDIWA)

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

9.1   MAJUKUMU YA KAZI

·         Kushughulikia upembuzi yakinifu, usanifu wa ujenzi, uendeshaji na matengenezo ya miundombinu midogo midogo ya usambazaji maji na kushiriki shughuli za upembuzi yakinifu, usanifu, ujenzi, uendeshaji na matengenezo ya miundombinu mikubwa ya ujenzi wa usambazaji maji na usafi wa mazingira.

·         Kufanyia mapitio taarifa za upembuzi yakinifu na sanifu za ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji maji na usafi wa mazingira.

·         Kufanyia ukaguzi wa utekelezaji wa ujenzi, uendeshaji na utengenezaji wa miundombinu ya uzalishaji na usambazaji maji na usafi wa mazingira kwa ajili ya kupata ubora unaokusudiwa.

·         Kushiriki katika kazi ya kupendekeza miradi na kupitia mapendekezo ya miradi (project proposal) ya usambazaji maji na usafi wa mazingira.

·         Kufanya uchunguzi kuhusu uharibifu wa miundombinu au ajali zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira.


·         Kutayarisha bajeti ya utekelezaji wa shughuli za sekta za maji.

·         Kusimamia kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa ujenzi, uendeshaji na mategenezo ya miundombinu ya miradi ya maji na usafi wa mazingira.

·         Kukusanya na kutayarisha taarifa mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za sekta ya maji kwa ajili ya matumizi ya sekta na kwa ajili ya kujisajili katika bodi ya Wahandisi.

9.2   SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye Shahada/Stashahada ya juu ya uhandisi wa Maji (Water Resource Engineering) kutoka vyuo vikuu vinavyotambuliwa na Serikali.

9.3   MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.


10.1      FUNDI SANIFU MSAIDIZI MITAMBO YA MAJI (UMEME) – NAFASI 15 (INARUDIWA)

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji.

10.1        MAJUKUMU YA KAZI

·         Kufanya kazi kwa kuongozwa na chini ya uangalizi wa Fundi sanifu aliyesajiliwa ili aweze;

·         Kufunga mfumo wa umeme unaohitajika kwa ajili ya uendeshaji wa mitambo ya miradi ya maji na usafi wa mazingira;

·         Kufunga mota na vifaa vingine vya umeme vya aina mbalimbali vya miradi ya maji na usafi wa mazingira;

·         Kufanya usafi na ukaguzi wa mfumo wa umeme, mota na vifaa vingine umeme vya miradi ya maji na usafi wa mazingira kwa ajili ya kukidhi uendeshaji nadhifu wa pampu na kuzuia uharibifu;

·         Kuendesha mitambo inayotumia umeme ya miradi ya maji na usafi wa mazingira;

·         Kufanya matengenezo ya kawaida, ya vipindi na ya kuzuia uharibifu kwenye mfumo wa umeme, mota na vifaa vingine umeme kwa kufuata miongozo ya uendeshaji, na inapohitajika kwa dharura.

·         Kunakili, kutayarisha, kukusanya, kutunza na kuziwasilisha takwimu za uendeshaji na matengenezo ya mitambo inayotumia umeme ya miradi ya maji na usafi wa mazingira;

·         Kumsaidia Fundi Sanifu katika kazi za kiufundi.


10.2        SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne waliohudhuria na kufaulu mafunzo ya mwaka mmoja kutoka Chuo cha Maji au Chuo chochote kinachitambuliwa na Serikali ambao wana Cheti cha ufundi Daraja III (Plants Technician Electrical).

10.3        MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.

11.0      FUNDI SANIFU MSAIDIZI (MAJI) (ASISTANT TECHNICIAN - WATER) NAFASI 24 (INARUDIWA)

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji.

11.1        MAJUKUMU YA KAZI
·         Kupima uwingi wa maji mtoni

·         Kusoma kituo cha hali ya hewa

·         Kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.

11.2        SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha VI waliohudhuria na kufaulu mafunzo ya mwaka mmoja kutoka kutoka Chuo cha Maji au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali ambao wana cheti cha ufundi Daraja la III katika fani ya maji.

11.3        MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.

12.1      MHANDISI KILIMO II (IRRIGATION) - 1

12.1        MAJUKUMU YA KAZI
·         Kuandaa programu za mafunzo kwa wakulima kutumia zana za kilimo.

·         Kushiriki katika kufundisha wakulima na matumizi bora ya zana.

·         Kushiri katika ujenzi wa miradi ya umwagiliaji.

·         Kushirikiana na mafundi sanifu kuwafundisha wakulima uendeshaji wa skimu za umwagiliaji.

·         Kukusanya takwimu za miradi ya umwagiliaji.

·         Kushiriki kuratibu na kutoa huduma za umwagiliaji kwa vikundi vya umwagiliaji pamoja na matumizi ya maji.

·         Kuandaa mafunzo/maonesha ya matumizi ya zana za kilimo.

·         Kufuatilia program za mafunzo ya wanyama kazi, mafundi wa matrekta na wakulima jinsi ya matumizi ya wanyama na matrekta.

·         Kuwafundisha wakulima jinsi ya ujenzi wa vihenge bora.

·         Kushughurikia ubora wa zana na kuwashauri waagizaji na watengenezaji ipasavyo.

12.2        SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye shahada ya uhandisi yenye mwelekeo mkubwa katika fani ya kilimo cha umwagiliaji kutoka chuo kikuu kinachotambuliwa na serikali.

12.3        MSHAHARA

·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi


13.0      MHANDISI KILIMO II (MECHANIZATION) – 1

13.1        MAJUKUMU YA KAZI
·         Kuandaa programu za mafunzo kwa wakulima kutumia zana za kilimo.

·         Kushiriki katika kufundisha wakulima na matumizi bora ya zana.

·         Kushiri katika ujenzi wa miradi ya umwagiliaji.

·         Kushirikiana na mafundi sanifu kuwafundisha wakulima uendeshaji wa skimu za umwagiliaji.

·         Kukusanya takwimu za miradi ya umwagiliaji.

·         Kushiriki kuratibu na kutoa huduma za umwagiliaji kwa vikundi vya umwagiliaji pamoja na matumizi ya maji.

·         Kuandaa mafunzo/maonesha ya matumizi ya zana za kilimo.

·         Kufuatilia program za mafunzo ya wanyama kazi, mafundi wa matrekta na wakulima jinsi ya matumizi ya wanyama na matrekta.

·         Kuwafundisha wakulima jinsi ya ujenzi wa vihenge bora.

·         Kushughurikia ubora wa zana na kuwashauri waagizaji na watengenezaji ipasavyo.

13.2        SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye shahada ya uhandisi yenye mwelekeo mkubwa katika fani ya zana za kilimo kutoka chuo kikuu kinachotambuliwa na serikali.

13.3        MSHAHARA
·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi

14.0      MHANDISI KILIMO II (LAND USE PLANNING) – 1

14.1        MAJUKUMU YA KAZI

·         Kuandaa programu za mafunzo kwa wakulima kutumia zana za kilimo.

·         Kushiriki katika kufundisha wakulima na matumizi bora ya zana.

·         Kushiri katika ujenzi wa miradi ya umwagiliaji.

·         Kushirikiana na mafundi sanifu kuwafundisha wakulima uendeshaji wa skimu za umwagiliaji.

·         Kukusanya takwimu za miradi ya umwagiliaji.

·         Kushiriki kuratibu na kutoa huduma za umwagiliaji kwa vikundi vya umwagiliaji pamoja na matumizi ya maji.

·         Kuandaa mafunzo/maonesha ya matumizi ya zana za kilimo.

·         Kufuatilia program za mafunzo ya wanyama kazi, mafundi wa matrekta na wakulima jinsi ya matumizi ya wanyama na matrekta.

·         Kuwafundisha wakulima jinsi ya ujenzi wa vihenge bora.



·         Kushughurikia ubora wa zana na kuwashauri waagizaji na watengenezaji ipasavyo.

14.2        SIFA ZA MWOMBAJI

·         Kuajiriwa wenye shahada ya uhandisi yenye mwelekeo mkubwa katika fani ya matumizi bora ya ardhi (land use planning) kutoka chuo kikuu kinachotambuliwa na serikali.

14.3        MSHAHARA

·         Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E wa mwezi

NB: MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.

i.       Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45

ii.       Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.

iii.      Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.

iv.       Nafasi ya kazi inayoombwa iandikwe juu ya bahasha, kutozingatiwa hili kutasababisha maombi ya kazi kuwa batili.

v.       Waombaji  waambatishe  maelezo  binafsi  yanayojitosheleza  (Detailed C.V)  yenye

anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.

vi.    Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Viambatanisho hivyo vibanwe sawa sawa kuondoa uwezekano wa kudondoka au kupotea.

-       Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.

-       Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI

-       Computer Certificate

-       Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)

-       Picha moja “Passport size” ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.



vii.      Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.

viii.      Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA).

ix.       Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.

x.       Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.

xi.       Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

xii.      Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 7 Febuari, 2015

xiii.      Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya ajira HAURUHUSIWI.

xiv.       Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza na yatumwe kupitia posta kwa anuani ifuatayo.




Katibu,
AU
Secretary,
Sekretariati ya Ajira katika

Public Service Recruitment
Utumishi wa Umma,

Secretariat,
SLP.63100,

P.O.Box 63100
Dar es Salaam.

Dar es Salaam.
TANGAZO LA KAZI UTUMISHI - KISWAHILI - 23 Januari, 2015 TANGAZO LA KAZI UTUMISHI - KISWAHILI - 23 Januari, 2015  Reviewed by Unknown on 8:32:00 AM Rating: 5

JOBS CATEGORY

Tanzania Kenya NGO JOBS Uganda Best Jobs Consultancy Rwanda ICT JOBS Administrative United Nations Sudan Best Jobs Finance Health - Medical Engineering Ethiopia Education Agricultural Lecturer Human Resources Somalia Media Congo - Kinshasa Legal Jobs Bank Jobs Monitoring and Evaluation Mining World Vision Burundi Procurement African Barrick Gold Accountant Zambia Sales and Marketing US EMBASSY East African Community Mozambique Telecoms Research CARE International Save The Children Plan International Arusha Malawi South Sudan Oxfam Scholarships African Development Bank Finance and Administration SafariCom Aviation The Commonwealth American Embassy Sales Zanzibar Environmental Catholic Relief Services Dar es salaam USAID Operations FHI 360 UNDP Security World Bank Economist TradeMark East Africa Unicef Hospitality Managers International Rescue Committee (IRC) Restless Development Accounting Civil Engineers AMREF Morogoro Utumishi AfDB African Development Bank COOPI - Cooperazione Internazionale Driver - Logistics Path International Mwanza African Union Tigo Jobs Marketing Mbeya Teaching Au African Union PSI Population Services International Pwc PricewaterhouseCoopers East African Breweries North Mara Gold Mine ACTED Djibouti Malaria Consortium Bulyanhulu Gold Mine DFID Driver Buzwagi Gold Mine Jhpiego COMESA FINCA JOBS International Jobs Adeso Danish Refugee Council Kilimanjaro Nairobi Coca-Cola Handicap International Pact International Rio Tinto Solidarités International Tender EGPAF Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation Logistics Serengeti Breweries Ltd Nation Media Group Africare Norwegian Refugee Council Samaritan's Purse Chemonics International COUNTRY DIRECTOR ICAP of Columbia University InterShips Precision Air RwandAir Marie Stopes International (MSI) Serengeti Breweries Volunteer Climate Change IGAD Tetra Tech ARD Agriculture Jobs Dodoma Iringa One Acre Fund Project Management Clinton Health Access Initiative (CHAI Technoserve Twaweza East Africa ActionAid Lutheran World Federation SADC Secretariat Tanga Vso International ACDI/VOCA Halmashauri Agha Khan Kenya Commercial Bank World Agroforestry Centre Deloitte East Africa International Organization for Migration (IOM) COMESA Secretariat: Software Engineering Safety and Security Shinyanga Jobs Tanzania Breweries Pathfinder International World Health Organization KPMG TANROADS Tanzania Electric Supply Company British Council Futures Group KCB BANK UN-Habitat WFP World Food Programme Barclays GEITA GOLD MINING TANESCO Electrical Engineer Food and Agriculture Organization GOAL Mombasa Tabora WWF World Wide Fund for Nature Microsoft Tanzania Ports Authority East African Development Bank Family Health International (FHI) IBM EAST AFRICA IntraHealth International Mercy Corps SERIKALINI - GOVERNMENT OF TANZANIA AccessBank Community Development Jobs Data Base Management Google Africa ICAP - TZ KEMRI/CDC Program WaterAid Tanzania Auditor SNV International Stanbic Bank Amnesty Horn Relief Kampala Management Systems International (MSI) Standard Chartered Bank VETA Christian Aid DIAMOND TRUST BANK Helen Keller International Help Age Mtwara Uganda Telecom Airtel Africa Equity Bank Internships Marie Stopes TCRA Web Development B B C WORLD SERVICE Human Rights Kigali Makerere University Nile Basin Initiative Kenyatta University Kigoma Mzumbe University NSSF National Social Security Fund Nile Breweries Limited Tulawaka Gold Mine University of Nairobi kenya Airways Bank of Tanzania Graduates MTN Muhimbili National Hospital Nepad Partners in Health Room to Read SUMATRA UNWOMEN African Wildlife foundation (AWF) KEMRI Kagera Librarian MENTOR Initiative Trainee USAILI - INTERVIEW Uiversity of Nairobi WaterAid International icipe Project CAFOD - Catholic Agency for Overseas Development Egerton University EngenderHealth Goal Ireland Kenyan Banks Lake Victoria Basin Commission Peace Corps TANAPA TASAF Tanzania Social Action Fund Zanzibar University ACB AKIBA COMMERCIAL BANK AGRA Alliance for a Green Revolution in Africa Advans Bank Ethiopian Airlines Freedom House IITA International Institute of Tropical Agriculture Legal Moshi NMB BANK Resolute Tanzania Singida Uganda Uganda National Roads Authority University of Dar es salaam University of Dodoma British High Commission ChildFund EWURA FilmAid International NECTA TPDC Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) United States International University World Concern Aga Khan Foundation CBA Commercial Bank of Africa Ecomist Ernst and Young IUCN International Union for Conservation of Nature International Medical Corps Islamic Relief Kakira Sugar Musoma National Institute for Medical Research OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA Relief International TAA Tanzania Airports Authority Trócaire Uganda Revenue Authority VODACOM TANZANIA VSF Belgium Architects Hivos IFC International Finance Corporation Ifakara Health Institute Inoorero University International Commercial Bank Kenya Red Cross Society MADEREVA Medical Oil and Gas Pwani University College SOKOINE UNIVERSITY Tumaini University Water Engineering AWF African Wildlife Foundation Acacia Mining Accounts African Virtual University Altima Africa Ardhi University Bank of Uganda Business Development Concultancy Del Monte Kenya Embassies Kenya Airports Authority Lake Victoria South Water Services Board Mara National Bank of Commerce RECORDS MANAGEMENT JOBS RUKWA Ruvuma Search for Common Ground Songea TTCL Tanzania Telecommunications Company Limited Unilever War Child International Zinduka Afrika ACORD AKU ​Aga Khan University Africa Nazarene University Africa Rice Center (AfricaRice) Aga Khan Health Services CRDB BANK Commercial Bank of Africa Daraja Tanzania Engineers Registration Board (ERB) Fina Bank International Potato Center International Potato Center (CIP) Intrahealth Jomo Kenyatta University Kilimanjaro Christian Medical Centre Kyambogo University Lindi Jobs MCL Mwananchi Communications MUHAS-harvad Moi University NBC BANK National University of Rwanda Ngorongoro Conservation Area Authority Njombe Nuru International Nzoia sugar Company RTI International SUA SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE THE LAW SCHOOL OF TANZANIA TRA Tanzania Revenue Authority Tanzania Postal Bank The Foundation For Civil Society Udhamini wa Masomo Western Union AIR TANZANIA Action Against Hunger (ACF) Agricultural Society of Kenya BRALIRWA Bondo University College Caritas Comoros Concern Worldwide Conservation Jobs Consolidated Bank of Kenya DHL Express Ewaso Ngiro South River Basin Development Authority Geologist Gulf African Bank INSTITUTE OF ADULT EDUCATION Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology Kabale University Kabale University (KAB) Kenya Ports Authority KickStart International MORUWASA Morogoro Urban Water and Sanitation Authority MSH Management Sciences for Health Mumias Sugar Company Nairobi Hospital Nkumba University Rural Electrification Agency SOKINE UNIVERSITY SONGWE STAMIGOLD Stores TACAIDS TARURA TCU Tanzania Commission for Universities Tullow Oil World Lung Foundation (WLF) ALAF Limited Aga Khan Development Network (AKDN) Aga Khan Hospital Air Malawi American Refuge Committee BENKI YA POSTA - TPB BANK BTC Belgian Technical Cooperation Bhttp://www.blogger.com/img/blank.gifank of Tanzania Bioversity International CHF International Customer Service Jobs DANGOTE DIT DAR ES SALAAM INSTITUTE OF TECHNOLOGY Danida Dar es Salaam Institute of Technology Daystar University ECOBANK ETDCO Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Company European Union IFM INSTITUTE OF FINANCE MANAGEMENT INSURANCE JOBS - BIMA ITECH Internews® Network KUITWA KAZINI Kenya Accreditation Service Kenya Polytechnic University College Kilombero Sugar Company Kisii University College Kisumu Laboratory Jobs MSD MEDICAL STORES DEPARTMENT MSF Switzerland Management Sciences for Health Manyara Maseno University Ministry of State for Planning Muteesa 1 Royal University Médecins Sans Frontières NIDA National Identification Authority Narok University College OSHA Occupational safety and Health Authority Open Society Initiative for Eastern Africa (OSIEA) PA PAC PEPSI POLICE - POLISI Petroleum EngineerS RWANDA HOUSING AUTHORITY Seychelles Songas TBC TANZANIA BROADCASTING CORPORATION TBS TANZANIA BUREAU OF STANDARDS TFDA TANZANIA FOOD AND DRUGS AUTHORITY TIB - Tanzania Investment Bank Tanzania Mortagage Refinance Company Tanzania Teachers’ Union Transmara Sugar Company Tropical Pesticides Research Institute Tumba College of Technology Twiga Cement UNESCO UNOCHA Umma University University WRP Walter Reed Project ZANTEL ao uga
Powered by Blogger.