Majibu ya Hoja za wadau kwa mwezi Oktoba na Novemba, 2014.

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, inapenda kuwashukuru wadau wote waliouliza maswali pamoja na kutuandikia maoni mbalimbali kwa njia ya simu na barua pepe kwa kipindi chote cha miezi miwili. 
Pia tunapenda kuwajulisha wale wote waliotuandikia maoni na maswali kwa kutumia baruapepe zao kuwa wazifungue kwani tulijibu kila swali na kuwatumia katika anwani husika, na baadae kuyaunganisha maswali na maoni yanayofanana na kuyatolea majibu ya jumla kwa faida ya wasomaji wetu wengine ili kuendelea kuelimishana kuhusu masuala yanayohusu mchakato wa ajira Serikalini. 
Aidha, tunapenda kukaribisha maoni na ushauri zaidi wenye kujenga chombo hiki na kuboresha huduma inayotolewa na chombo hiki ili kuhakikisha Serikali inaendelea kuajiri Watumishi wa Umma ambao wana sifa na vigezo stahili vya kuajiriwa Serikalini na walio tayari kuwatumikia wananchi.
Swali la 1.
Habari,  naomba kufahamu, nyie tume mnatoa nafasi za udereva mara kwa mara.je unapotuma barua mara moja inatosha au inabidi utume kila unapoona nafasi imetangazwa? Kwa sababu nimeshatuma barua zaidi ya 7, lakini kila ninapoingia kwenye mtandao naona nafasi za udereva barua zitumwe kupitia tume ya utumishi.sasa naomba msaada wako, kazi njema.
Jibu.
Tunashukuru kwa swali lako la kutaka ufafanuzi, Ni kweli hivi karibuni Sekretarieti ya Ajira imekuwa ikitangaza nafasi mbalimbali za kazi mara kwa mara zikiwemo za udereva. Tunapenda kukufahamisha kuwa kila unapoona tangazo la kazi linatokana na mahitaji ya waajiri ni tofauti, hivyo haikuzuii kuomba mara nyingi uwezavyo lakini pia tunakushauri ukishatuma maombi yako uwe unafuatilia mara kwa mara kwenye tovuti yetu ya www.ajira.go.tz  ili kufahamu wakati waombaji wanapoitwa kwenye usaili kwa kuwa tayari umeshatuma maombi mengi. Jambo la msingi wakati wa kutuma maombi yako ya kazi hakikisha unaweka viambatanisho vyote vinavyohitajika kwa mujibu wa tangazo la kazi ili uweze kukidhi mahitaji ya tangazo na kazi husika.
Swali la 2.
Naitwa IGNATUS J KAJORO nimeshafanya interview mara 4 za Supplies Assistant na Assistant Procurement and logistics officer baada ya hapo nikapigiwa simu kwa namba ya ttcl +255222153517 lakini sikuweza kupokea simu badae nilifuatilia nikaambiwa nilikuwa naitwa kazini. Pia nikaambiwa nitapigiwa simu pindi nafasi zikipatikana lakini mpaka sasa sijapigiwa simu tena na niko kwenye kazidata. Naomba kujua ni lini nitaitwa kuja kuchukua barua ya kuitwa kazi. wako mtiifu, asante mungu awabariki kazi njema.
Jibu.
Nakupa pole kwa jambo hilo inawezekana ni kweli ulipigiwa simu mara kadhaa lakini hukuweza kupokea simu au hukupatikana hewani kama ulivyoeleza na kupelekea nafasi yako kupangiwa mtu mwingine, Aidha kwa kuwa upo kwemye kanzidata tunaendelea kukushauri kuvuta subira na endapo itapatikana nafasi nyingene ya kazi  utajulishwa kama ulivyofahamishwa hapo awali.  Pamoja na kuvuta subira ni vizuri ukafahamu pia kuwa matumizi ya kanzidata yana muda maalum na pale muda unapokwisha utaratibu huanza upya. Aidha tunakushauri kuhakikisha simu yako inakuwa hewani muda wote ili isije ikatokea ukakosa fursa nyingine.
Swali la 3.
habari! jina langu ni Farida Hamis, nimechaguliwa kujiunga na TBC lakini sijatumiwa barua mpaka sasa, je naweza kuripoti bila barua?
Jibu
Asante kwa swali lako,Jibu ni kwamba kama ulifaulu usaili na kupangiwa kituo cha kazi barua yako yako itakuwa imeshatumwa kwenye anuani uliyotumia wakati wa maombi ya kazi, Aidha kama hadi sasa hujapata barua hiyo unapaswa  kufika Ofisi za Sekretarieti ya ajira kwa ajili ya msaada zaidi.
Swali la 4.
Habari za majukumu, poleni na ubize wa kazi,naomba kufahamishwa ni lini watu wa supplies assistant kule gpsa wataitwa kazini..nategemea sana majibu yenu.
asanteni
Jibu.
Asante kwa swali lako waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kuanzia tarehe 21Oktoba hadi tarehe 05 Novemba, 2014 wakiwemo watu wa Supplies Assistant  wa GPSA tangazo la kupangiwa/kuitwa kazini lilishatolewa tangu tarehe 20 Novemba, 2014 hivyo tunakushauri kuangalia tangazo hilo katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira www.ajira.go.tz.
Swali la 5.
Naomba msaada kwa hiyo chuo cha ilemi polytechnic college ndo hataomba tena ajira.na je tufanyeje hapa sasa kuhusu mstakabari wa maisha?
Jibu.
Kuhusu chuo cha Ilemi Polytecnic college tunachoweza kukujibu ni kwamba hakikuwa miongoni mwa vyuo vinavyotambuliwa na Wizara ya Kilimo, chakula na Ushirika lakini kinatambuliwa na Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi stadi (VETA) hivyo Sekretarieti ya Ajira bado inafanya mawasiliano na Wizara husika na taarifa kuhusu wahitimu wanaomba ajira na wamesoma katika chuo hicho, watapewa taarifa baada ya kupata muongozo wa Wizara husika.
Swali la 6.
Mimi naitwa samwel mhadisa nilimaliza chuo kikuu cha Dar es saalam mwaka2013 katika bachelor of science general (specialing applied microbiology with chemistry) sasa nilikuwa naomba unipe nafasi ya kuja kuonana na wewe hapo ofisini kwako na mimi sasa hivi nipo hapa Dar es salaam.nitashukru sana endapo ukinipa nafasi hii ya kuja kuzungumza na wewe
Jibu.
Ombi lako limepokelewa, Sekretarieti ya Ajira ni Taasisi ya serikali hivyo haina kizuizi kwa mwananchi yoyoye kufika kwa ajili ya kutaka kupata ufafanuzi wa jambo lolote linalohusiana na mchakato wa ajira serikalini, hivyo hata kama hutampata katibu wa Sekretarieti ya ajira wakati mwingine kutokana na majukumu yake unaweza kukutana na wasaidizi wake ambao pia unaweza kuonana nao na kukupatia ufafanuzi unaouhitaji.
Swali la 7.
 Kutofautiana majina, asante kwa kazi ngumu mnayoifanya ya kutoa maelekezo kwetu sisi wadau wa secretariat ya utumishi. Mimi cheti cha form four nilitumia majina mawili yaani AMANI JONAS, lakini chuoni liliongezeka jina la tatu yaani AMANI JONAS NYABUZOKI
Kwa hiyo natakiwa kwenda kuapa mahakamani au? kwani hilo jina la tatu ni ubini na liko pia kwenye cheti cha kuzaliwa. Natumaini nitapata majibu sahihi. Asante na kazi njema.
Jibu.
Asante kwa kuuliza swali hili, kwa kuwa cheti cha kumaliza kidato cha nne kina majina mawili tu yaani (Amani Jonas) wakati vyeti vingine vya kitaaluma na cha kuzaliwa vinasomeka kwa majina ya Amani Jonas Nyabuzoki hapo tayari  utaona kuna utofauti wa majina na mtu anaweza kudhani ni watu wawili tofauti, Hivyo unashauriwa kwenda mahakamani kuapa (Deed Poll) na utapewa hati inayokutambulisha kwamba majina katika vyeti hivyo yote ni ya kwako.
Swali la 8.
Nauliza hivi karibuni nilituma maombi kwenye zile nafasi 100 za NAO. Jina langu halijatoka ktk majina ya usaili. Je Inawezekana ni kwa sababu niliweka transcript peke Yake? Na kuna mchujo huwa unafanyika kabla ya interview? Mwisho kwenye bahasha yangu natakiwa kuandika post ninayoomba kwa mbele au nyuma ya bahasha? Kazi njema. Joshua Mchiwa, mbeya.
Jibu.
Ni kweli hivi karibuni nafasi hizo ulizotaja zilitangazwa na tayari walioomba kazi baada ya kufanya usaili na kufaulu tayari walishapangiwa vituo vya kazi, swala la jina lako kutotokea katika orodha ya walioitwa kwenye usaili inawezekana ni kutokana na sababu mbalimbali ambazo zinakufanya usikidhi vigezo ikiwemo uliyoitaja hapo juu kwa kuwa Transcript pekee haitoshi kwa kuwa ni lazima iwe pamoja na cheti chake isipokuwa kama umemaliza mwaka huu na cheti bado hakijatoka ndio unaweza kutumia transcript wakati wa kuomba kazi. Swali lako la pili nafasi unayoomba unatakiwa kuandika juu na mbele ya bahasha.
Swali la 9.
Waliopotelewa na vyeti vya taaluma wanapoomba kazi serikalini
Ndugu Katika mamlaka ya ajira Tanzania. Kutokana natangazo la hivi karibuni linalo eleza mambo ya kuzingatia Mimi ni Hemed A. Kavumo mmoja wa watu waliopotelewa na cheti cha form four na nimefanya taratibu zote na Necta na wakadai wameshatuma taarifa zangu tume ya ajira, tatizo ni kwamba sinahakika kua taarifa hizo zimewafikia tume ya ajira. 
Wakati wa kuomba kazi kwa walio potelewa na vyeti napenda kuuliza maswali ya fuatayo.
Mtu aliye potelewa na cheti nakuripoti necta na akaambiwa taarifa zake zitatumwa nivipi atajua kama taarifa zake zakupotelewa na cheti zimewafikia tume ya ajira pindi anapo omba kazi?
Pili ni nanma gani tume ya ajira itafahamu kuwa mtu flani amepotelewa na cheti na sio kuwa hakutimiza vigezo au viambatanisho pindi anapoomba kazi serikalini?
Ushauri wangu ni kwamba aliyepotelewa na cheti na kutoa taarifa kwenye mamlaka husika na taarifa zake kutumwa mamlaka ya ajira apewe majibu kua taarifa zake zakupotelewa na cheti zimefika tume ya ajira na anapoomba kazi aandike barua kueleza kua taarifa za kupotelewa na cheti husika zimeshaifikia tume ya ajira ili kuepusha usumbufu na kuwezesha tume ya ajira ihakiki taarifa hizo. 
Ahsante.
Jibu.
Tumepokea maswali yako, awali ya yote nikupe pole kwa kupotelewa na cheti cha kidato cha nne, Aidha ni kweli kwamba baadhi ya watu waliopotelewa na vyeti vya kidato cha nne na sita wanapoenda kuripoti Baraza la Mitihani (NECTA) juu ya upotevu wa vyeti vyao na wakaomba taarifa za kupoteza vyeti vyao zitumwe Sekretarieti ya Ajira utaratibu huo huwa unafanyika.
A)    Kama ulipoteza cheti ukaripoti NECTA na ukawaomba taarifa zako wazitume Sekretarieti ya Ajira ili kufahamu unapaswa kuwasiliana na Sekretarieti ya ajira ili kuulizia kama jina lako limefika(unaweza kupiga simu kwa namba hii 0687 624975 au tuma ujumbe kwenye ukurasa wetu wa facebook www.facebook.com/sekretarieti ajiara). Pia unapoitwa kwenye usaili siku ya usaili kabla ya kufanya usaili ni vyema ukauliza ili jina lako liangaliwe kwenye orodha yetu tuliyoipata kutoka NECTA kujiridhisha kabla hujaingia kwenye usaili.
B)    Sekretarieti ya ajira itafahamu kuwa mtu fulani amepotelewa cheti kwa kupata taarifa au jina kutoka mamlaka husika inayotoa cheti baada ya aliyepoteza cheti kutoa taarifa na kuomba jina lake litumwe sekretarieti ya ajira kama nilivyoeleza hapo awali.
C)    Ushauri wako umepokelewa lakini pia unakumbushwa kufuata maelekezo yaliyopo katika maelezo ya awali katika jibu la kipengele (a) ili kujiepushia usumbufu usiokuwa na lazima ikiwemo kupunguza gharama.
Swali la 10.
Habari za kazi, hivi mlitangaza nafasi za kazi katika wizara ya mambo ya nje ya receptionist na wahudumu wa ofisi, hivi mlishatoa majina ya watu watakaoenda kwenye usaili?
Jibu.
Ni kweli nafasi ya mapokezi (receptionist) pamoja na kada nyingine zilitangazwa hivi karibuni katika tovuti ya Sekretarieti ya ajira, Tangazo lenye orodha ya waombaji wanaoitwa kwenye usaili wa kada hizo na nyinginezo tayari limetolewa tangu tarehe 6 Desemba, 2014.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma 8 Desemba, 2014.
Majibu ya Hoja za wadau kwa mwezi Oktoba na Novemba, 2014. Majibu ya Hoja za wadau kwa mwezi Oktoba na Novemba, 2014. Reviewed by Unknown on 8:27:00 AM Rating: 5

JOBS CATEGORY

Tanzania Kenya NGO JOBS Uganda Best Jobs Consultancy Rwanda ICT JOBS Administrative United Nations Sudan Best Jobs Finance Health - Medical Engineering Ethiopia Education Agricultural Lecturer Human Resources Somalia Media Congo - Kinshasa Legal Jobs Bank Jobs Monitoring and Evaluation Mining World Vision Burundi Procurement African Barrick Gold Accountant Zambia Sales and Marketing US EMBASSY East African Community Mozambique Telecoms Research CARE International Save The Children Plan International Arusha Malawi South Sudan Oxfam Scholarships African Development Bank Finance and Administration SafariCom Aviation The Commonwealth American Embassy Sales Zanzibar Environmental Catholic Relief Services Dar es salaam USAID Operations FHI 360 UNDP Security World Bank Economist TradeMark East Africa Unicef Hospitality Managers International Rescue Committee (IRC) Restless Development Accounting Civil Engineers AMREF Morogoro Utumishi AfDB African Development Bank COOPI - Cooperazione Internazionale Driver - Logistics Path International Mwanza African Union Tigo Jobs Marketing Mbeya Teaching Au African Union PSI Population Services International Pwc PricewaterhouseCoopers East African Breweries North Mara Gold Mine ACTED Djibouti Malaria Consortium Bulyanhulu Gold Mine DFID Driver Buzwagi Gold Mine Jhpiego COMESA FINCA JOBS International Jobs Adeso Danish Refugee Council Kilimanjaro Nairobi Coca-Cola Handicap International Pact International Rio Tinto Solidarités International Tender EGPAF Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation Logistics Serengeti Breweries Ltd Nation Media Group Africare Norwegian Refugee Council Samaritan's Purse Chemonics International COUNTRY DIRECTOR ICAP of Columbia University InterShips Precision Air RwandAir Marie Stopes International (MSI) Serengeti Breweries Volunteer Climate Change IGAD Tetra Tech ARD Agriculture Jobs Dodoma Iringa One Acre Fund Project Management Clinton Health Access Initiative (CHAI Technoserve Twaweza East Africa ActionAid Lutheran World Federation SADC Secretariat Tanga Vso International ACDI/VOCA Halmashauri Agha Khan Kenya Commercial Bank World Agroforestry Centre Deloitte East Africa International Organization for Migration (IOM) COMESA Secretariat: Software Engineering Safety and Security Shinyanga Jobs Tanzania Breweries Pathfinder International World Health Organization KPMG TANROADS Tanzania Electric Supply Company British Council Futures Group KCB BANK UN-Habitat WFP World Food Programme Barclays GEITA GOLD MINING TANESCO Electrical Engineer Food and Agriculture Organization GOAL Mombasa Tabora WWF World Wide Fund for Nature Microsoft Tanzania Ports Authority East African Development Bank Family Health International (FHI) IBM EAST AFRICA IntraHealth International Mercy Corps SERIKALINI - GOVERNMENT OF TANZANIA AccessBank Community Development Jobs Data Base Management Google Africa ICAP - TZ KEMRI/CDC Program WaterAid Tanzania Auditor SNV International Stanbic Bank Amnesty Horn Relief Kampala Management Systems International (MSI) Standard Chartered Bank VETA Christian Aid DIAMOND TRUST BANK Helen Keller International Help Age Mtwara Uganda Telecom Airtel Africa Equity Bank Internships Marie Stopes TCRA Web Development B B C WORLD SERVICE Human Rights Kigali Makerere University Nile Basin Initiative Kenyatta University Kigoma Mzumbe University NSSF National Social Security Fund Nile Breweries Limited Tulawaka Gold Mine University of Nairobi kenya Airways Bank of Tanzania Graduates MTN Muhimbili National Hospital Nepad Partners in Health Room to Read SUMATRA UNWOMEN African Wildlife foundation (AWF) KEMRI Kagera Librarian MENTOR Initiative Trainee USAILI - INTERVIEW Uiversity of Nairobi WaterAid International icipe Project CAFOD - Catholic Agency for Overseas Development Egerton University EngenderHealth Goal Ireland Kenyan Banks Lake Victoria Basin Commission Peace Corps TANAPA TASAF Tanzania Social Action Fund Zanzibar University ACB AKIBA COMMERCIAL BANK AGRA Alliance for a Green Revolution in Africa Advans Bank Ethiopian Airlines Freedom House IITA International Institute of Tropical Agriculture Legal Moshi NMB BANK Resolute Tanzania Singida Uganda Uganda National Roads Authority University of Dar es salaam University of Dodoma British High Commission ChildFund EWURA FilmAid International NECTA TPDC Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) United States International University World Concern Aga Khan Foundation CBA Commercial Bank of Africa Ecomist Ernst and Young IUCN International Union for Conservation of Nature International Medical Corps Islamic Relief Kakira Sugar Musoma National Institute for Medical Research OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA Relief International TAA Tanzania Airports Authority Trócaire Uganda Revenue Authority VODACOM TANZANIA VSF Belgium Architects Hivos IFC International Finance Corporation Ifakara Health Institute Inoorero University International Commercial Bank Kenya Red Cross Society MADEREVA Medical Oil and Gas Pwani University College SOKOINE UNIVERSITY Tumaini University Water Engineering AWF African Wildlife Foundation Acacia Mining Accounts African Virtual University Altima Africa Ardhi University Bank of Uganda Business Development Concultancy Del Monte Kenya Embassies Kenya Airports Authority Lake Victoria South Water Services Board Mara National Bank of Commerce RECORDS MANAGEMENT JOBS RUKWA Ruvuma Search for Common Ground Songea TTCL Tanzania Telecommunications Company Limited Unilever War Child International Zinduka Afrika ACORD AKU ​Aga Khan University Africa Nazarene University Africa Rice Center (AfricaRice) Aga Khan Health Services CRDB BANK Commercial Bank of Africa Daraja Tanzania Engineers Registration Board (ERB) Fina Bank International Potato Center International Potato Center (CIP) Intrahealth Jomo Kenyatta University Kilimanjaro Christian Medical Centre Kyambogo University Lindi Jobs MCL Mwananchi Communications MUHAS-harvad Moi University NBC BANK National University of Rwanda Ngorongoro Conservation Area Authority Njombe Nuru International Nzoia sugar Company RTI International SUA SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE THE LAW SCHOOL OF TANZANIA TRA Tanzania Revenue Authority Tanzania Postal Bank The Foundation For Civil Society Udhamini wa Masomo Western Union AIR TANZANIA Action Against Hunger (ACF) Agricultural Society of Kenya BRALIRWA Bondo University College Caritas Comoros Concern Worldwide Conservation Jobs Consolidated Bank of Kenya DHL Express Ewaso Ngiro South River Basin Development Authority Geologist Gulf African Bank INSTITUTE OF ADULT EDUCATION Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology Kabale University Kabale University (KAB) Kenya Ports Authority KickStart International MORUWASA Morogoro Urban Water and Sanitation Authority MSH Management Sciences for Health Mumias Sugar Company Nairobi Hospital Nkumba University Rural Electrification Agency SOKINE UNIVERSITY SONGWE STAMIGOLD Stores TACAIDS TARURA TCU Tanzania Commission for Universities Tullow Oil World Lung Foundation (WLF) ALAF Limited Aga Khan Development Network (AKDN) Aga Khan Hospital Air Malawi American Refuge Committee BENKI YA POSTA - TPB BANK BTC Belgian Technical Cooperation Bhttp://www.blogger.com/img/blank.gifank of Tanzania Bioversity International CHF International Customer Service Jobs DANGOTE DIT DAR ES SALAAM INSTITUTE OF TECHNOLOGY Danida Dar es Salaam Institute of Technology Daystar University ECOBANK ETDCO Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Company European Union IFM INSTITUTE OF FINANCE MANAGEMENT INSURANCE JOBS - BIMA ITECH Internews® Network KUITWA KAZINI Kenya Accreditation Service Kenya Polytechnic University College Kilombero Sugar Company Kisii University College Kisumu Laboratory Jobs MSD MEDICAL STORES DEPARTMENT MSF Switzerland Management Sciences for Health Manyara Maseno University Ministry of State for Planning Muteesa 1 Royal University Médecins Sans Frontières NIDA National Identification Authority Narok University College OSHA Occupational safety and Health Authority Open Society Initiative for Eastern Africa (OSIEA) PA PAC PEPSI POLICE - POLISI Petroleum EngineerS RWANDA HOUSING AUTHORITY Seychelles Songas TBC TANZANIA BROADCASTING CORPORATION TBS TANZANIA BUREAU OF STANDARDS TFDA TANZANIA FOOD AND DRUGS AUTHORITY TIB - Tanzania Investment Bank Tanzania Mortagage Refinance Company Tanzania Teachers’ Union Transmara Sugar Company Tropical Pesticides Research Institute Tumba College of Technology Twiga Cement UNESCO UNOCHA Umma University University WRP Walter Reed Project ZANTEL ao uga
Powered by Blogger.