WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzaia
umeanzishwa kwa mujibu wa Kifungu Na.245 cha Sheria ya Wakala ya Mwaka 1997 na
kutangazwa rasmi kufuatia Tangazo la Serikali Na.269 la tarehe 30/07/2010.
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania umechukua kazi na majukumu ya iliyokuwa
Idara ya Misitu na Nyuki.
1.1
AFISA MISITU DARAJA LA II –NAFASI 1
1.1.1 MAJUKUMU YA KAZI
·
Kusimamia
upandaji na uhudumiaji wa miti na misitu
·
Kusimamia
uendeshaji wa misitu ya kupandwa isiyozidi hekta 5,000 au asili isiyozidi hekta
10,000
·
Kufanya
utafiti wa misitu
·
Kutekeleza
Sera na Sheria za misitu
·
Kuendesha
mafunzo ya Wasaidizi Misitu
·
Kukusanya
takwimu za misitu
·
Kufanya
ukaguzi wa misitu
·
Kupanga
na kupima madaraja ya mbao
·
Kuthibiti
leseni na uvunaji wa miti
·
Kutoa
ushauri na mafunzo kwa wananchi juu ya uendeshaji na matumizi endelevu ya miti
na misitu kwa wananchi
·
Kufanya
ukadiriaji wa rasilimali za misitu
·
Kupima
maeneo na kuchora ramani za misitu
1.1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
· Kuajiriwa wenye Shahada ya Misitu
kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine au Vyuo Vikuu vingine vinavyotambuliwa
na Serikali.
1.1.3 MSHAHARA
· Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya
Serikali yaani TGS D
MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.
i. Waombaji wote wawe ni Raia wa
Tanzania.
ii. Waombaji wote waambatishe cheti cha
kuzaliwa.
iii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa
Umma na wamejipatia sifa za kuingilia katika kada tofauti na walizonazo,
wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na Waajiri
wajiridhishe ipasavyo.
iv. Nafasi ya kazi inayoombwa iandikwe
katika kichwa cha habari cha barua na juu ya bahasha, kutozingatiwa hili
kutasababisha maombi ya kazi kuwa batili.
1
v. Waombaji waambatishe maelezo binafsi
yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika
pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
vi.
|
Maombi
|
yote
yaambatane na vyeti
vya taaluma, maelezo,
nakala za vyeti
vya
|
|
|
kidato cha
nne na kidato
cha sita
|
kwawale waliofikia
kiwango hicho na
vyeti vya
|
|
|
kuhitimu
|
mafunzo mbalimbali kwa
|
kuzingatia
sifa za kazi
husika. Viambatanisho
|
|
hivyo vibanwe sawa sawa kuondoa uwezekano wa kudondoka
kupotea.
|
-
Postgraduate/Degree/Advanced
Diploma/Diploma/Certificates.
-
Cheti
cha mtihani wa kidato cha IV na VI
-
Computer
Certificate
-
Vyeti
vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
-
Picha
moja “Passport size” ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
viii. “Transcripts”, “Testmonials”,
“Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne
na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
ix.
Waombaji
wawe na umri usiozidi miaka 45.
x. Waombaji waliostaafishwa katika
Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu
Kiongozi.
xi. Waombaji kazi ambao tayari ni
waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika utumishi wa umma wasiombe
na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140
wa tarehe 30 Novemba 2010.
xii. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za
kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
xiii. WAAJIRI WOTE WALIOPO NJE YA DAR ES
SALAAM WANAOMBWA KUSAMBAZA MATANGAZO HAYA KWENYE MBAO ZA MATANGAZO NA MAENEO
MENGINE.
xiv. Mwisho wa kupokea barua za maombi ni
tarehe 2 May, 2013
xv. Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono
katika ofisi za Sekretarieti ya ajira HAURUHUSIWI.
xvi. Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya
Kiswahili au Kiingereza na yatumwe kupitia posta kwa anuani ifuatayo.
Katibu,
|
AU
|
Secretary,
|
Sekretariati ya Ajira katika
|
|
Public Service Recruitment
|
Utumishi wa Umma,
|
|
Secretariat,
|
SLP.63100,
|
|
P.O.Box 63100
|
Dar es Salaam.
|
|
Dar es Salaam.
|
AFISA MISITU DARAJA LA II
Reviewed by Unknown
on
3:53:00 AM
Rating: