27 Julai, 2012
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi ya
Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi za kazi 79 mbalimbali kwa Waajiri
(Taasisi za Umma) kama ilivyoorodheshwa hapa chini:
1.0 WAKALA WA VIPIMO
Wakala wa Vipimo ni Taasisi (Wakala) ya Serikali iliyo chini ya Wizara ya Viwanda na
Biashara. Taasisi hii iliundwa kwa mujibu wa Sheria za Serikali Sura Na. 245, mapitio ya
mwaka 2002. Wakala wa Vipimo ilianzishwa rasmi tarehe 13 Mei, 2002 kwa amri ya
Seriakali Na. 194 (Government Order No. 194) na kutangazwa tarehe 17 Mei, 2002. Chini
ya sheria hiyo, Wakala wa Vipimo ina jukumu la kumlinda malaji Kwa kuhakiki vipimo vyote
vinavyotumika katika sekta za Biashara, Afya, Usalama na Mazingira.
1.1 AFISA VIPIMO II – NAFASI 6
1.1.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kukagua, kuhakiki na kuvirekebisha vipimo vya wafanyabiashara;
•Kutunza, kuhifadhi vifaa vya kitaalam vitumikavyo katika utendaji wa kazi;
•Kutoa ushauri kuhusu masuala ya uhakiki na matumizi ya vipimo;
•Kufanya upelelezi kuhusu ukiukwaji wa Sheria ya Vipimo
•Kupokea na kufanyia kazi malalamiko ya wadau na waateja;
•Kufanya kazi nyingine kama atakavyopangiwa na kiongozi wake zinazohusiana na
elimu na ujuzi wa kazi
1
1.1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza katika fani ya “Legal Metrology” au “Legal and
Industrial Metrology” toka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali. Au
•Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza ya Uhandisi/Sayansi ambao wamepata “Crash
programme” ya “Legal and Industrial Metrology” isiyopungua miezi mnne (4) toka
Chuo kinachotambuliwa na Serikali.
•Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza ya Uhandisi/Sayansi ambao wamehitimu
Stashahada ya Uzamili (Postgraduate Diploma) katika fani ya vipimo katika Chuo
kinachotambuliwa na Serikali.
•Kuajiriwa wenye Stashahada ya juu katika fani ya “Legal Metrology” /Legal and
“Industrial Metrology” toka Chuo kinachotambuliwa na Serikali.
1.1.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani PTSS 13 -14 kwa mwezi.
2.0MKUFUNZI MWANDAMIZI DARAJA II - NAFASI 1
Nafasi hii ni kwa ajili ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA)
2.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kufundisha wanafunzi wa mwaka 3 (NTA level 6)
•Kusimamia mitihani ya wanafunzi wa mwaka wa 3
•Kutayarisha na kuhuisha Mitaala ya chuo
•Kusimamia mafunzo ya vitendo
•Kusimamia wanafunzi walioko chini yake
•Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa Idara
2.2
SIFA ZA MWOMBAJI
•Shahada ya Uzamili katika fani Sanaa za Ufundi na Sanaa za Maonyesho (Muziki)
•Awe amesajiliwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Vyuo vya Ufundi (NACTE) mwenye
uzoefu wa kazi wa miaka mitatu (3).
2.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani PTSS 13 -14 kwa mwezi.
3.0
DEREVA MASHUA/VIVUKO DARAJA LA II (FERRY/ BOAT OPERATOR GRADE
II) - NAFASI 3
Nafasi hii ni kwa ajili ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA)
3.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kufunga na kufungua kamba za mashua/kivuko.
•Kuchunga usalama nwa abiria na magari yaliyomo ndani ya mashua/vivuko.
•Kupanga abiria au magari kwenye mashua/kivuko.
2
•
•
•
•
3.2
Kuendesha na kuongoza mashua/kivuko.
Kutunza daftari za safari ya mashua/kivuko.
Kuhakikisha kwamba injini za kivuko zipo katika hali nzuri ya kufanya kazi.
Kuangalia mafuta na vyombo vingine vya kufanyia kazi.
SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa waliohitimu Mtihani wa Kidato cha IV, wenye Ujuzi wa kuendesha na
kutunza Mashua/Kivuko uliothibitishwa na Chuo cha Dar es Salaam Marine Institute
au Chuo kingine chochote kinachotambuliwa na Serikali kwa muda usiopungua
miaka miwili; na waliofuzu mafunzo ya miezi sita ya uokoaji wa maisha majini,
kuogelea na kupanga watu na magari kwenye mashua/vivuko.
3.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGOS.A kwa mwezi
4.0 MPISHI DARAJA LA II (COOK GRADE II) – NAFASI 9
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Wizara ya
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halmashauri ya Manipsaa ya Mtwara na Taasisi
ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA)
4.1MAJUKUMU YA KAZI
•Kusafisha jiko
•Kupika chakula cha kawaida
4.2
SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha IV waliofuzu mafunzo ya cheti yasiyopungua
mwaka mmoja katika fani ya ‘Food Production’ yanayotolewa na Vyuo vya Forodhani
(Dar es Salaam), Masoka (Moshi), Arusha Hotel, Y.M.C.A (Moshi), VETA (Mikumi) na
Vision Hotel (Dar es Salaam) au vyeti vingine vitakavyotambuliwa na Serikali na
wenye uzoefu wa kazi kwa muda usiopunguja miaka (5) mitatu.
4.3MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi
5.0 MKUFUNZI DARAJA LA II – UCHENJUAJI MADINI MIGODI (TUTOR GRADE II)
NAFASI 2
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini
5.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kutafsiri mihutasari ya mafunzo kwenye masomo.
•Kuandaa mtiririko wa kila somo (lesson plan) kwa upande wa nadharia na vitendo
•Kufundisha kozi za stashahada na astashahada kwa upande wa nadharia na vitendo
•Kuandaa na kupanga somo la vitendo na kusimamia wanachuo wakati wa kujifunza.
3
•
•
•
Kupima maendeleo ya wanachuo kwenye mitihani kwa kipindi chote kinachohusika
na kutunza alama zao
Kupima maendeleo ya wanachuo kwa kushirikiana na wahandisi wa uchenjuaji/
jiolojia na wahandisi wa migodi wa viwandani wakati wa mafunzo kwa vitendo (field
practiclas)
Kufanya kazi nyingine kulingana na kiwango cha elimu kulingana na fani yake kadri
atakavyopangiwa na mkuu wake wa kazi.
5.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza katika fani ya Sayansi ya Uhandisi wa
Uchenjuaji Madini, Jiolojia au uhandisi Migodi kutoka chuo kinachotambuliwa na
Serikali na wenye uzoefu wa kazi usiopungua miaka mitatu.
5.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
6.0 MKUFUNZI MSAIDIZI (TUTORIAL ASSISTANT) – NAFASI 1
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini
6.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kuandaa mtiririko (lesson plan) wa somo
•Kufundisha kozi YA astashahada ya uchenjuaji madini, jiolojia na utafutaji wa madini
na uhandisi migodi
•Kusimamia maso mo ya vitendo chini ya usimamizi wa Mkufunzi Mkuu wa somo
•Kuandaa na kupanga vifaa kwa ajili ya somo la vitendo
•Kuwapima wanachuo wakati wa mazoezi ya somo la vitendo
•Anaweza kuteuliwa kuwa Mkuu wa kitengo (maabara, karakana na museum n.k)
•Kufanya kazi nyingine kulingana na kiwango cha elimu kulingana na fani yake kadri
atakavyopangiwa na mkuu wake wa kazi.
6.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne (IV) au sita (VI) waliofuzu mafunzo ya
Stashahada ya Uhandisi wa Uchenjuaji Madini, Jiolojia au uhandisi Migodi kutoka
chuo kinachotambuliwa na Serikali
6.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
4
7.0 FUNDI SANIFU DARAJA LA II - (TECHNICIAN GRADE II - PLUMBING) – NAFASI
20
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
7.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kufanya kazi za ufundi bomba atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi
7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye mojawapo ya sifa zilizotajwa hapa chini:
•Waliohitimu kidato cha VI na kufuzu mafunzo ya ufundi ya miaka miwili kutoka Chuo
kinachotambuliwa na Serikali katika fani ya fundi bomba (Plumbing)
•Waliohitimu kidato cha IV na kufuzu kozi ya ufundi bomba ya miaka mitatu kutoka
Vyuo vya Ufundi vinavyotambuliwa na Serikali katika mojawapo ya fani za ufundi,
•Wenye Cheti cha Majaribio ya Ufundi hatua ya I kutoka Chuo cha Ufundi
kinachotambuliwa na Serikali
•Wenye Stashahada ya Kawaida katika fani za ufundi bomba kutoka Chuo
kinachotambuliwa na Serikali.
7.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi
8.0 FUNDI SANIFU DARAJA LA II - (TECHNICIAN GRADE II – COMMUNITY
DEVELOPMENT) – NAFASI 7
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Manispaa ya Singida, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni,
Pangani, Halmashauri ya Jiji la Mwanza
8.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kufundisha wanavijiji teknolojia na ufundi
•Ujenzi wa nyumba bora za gharama nafuu
•Kusimamia utengenezaji wa majiko bora , ufinyanzi, uhunzi na useremla
•Utengenezaji wa nyenzo za usafiri kama mikokoteni, uchimbaji wa visima, ujenzi wa
vyoo bora, ujenzi wa mabanda na usimikaji wa mashine za kusaga
•Kusaidia, kuanzisha na kutoa ushauri wa kiufundi kwa vikundi vya ujenzi
•Kuratibu shghuli za ufundi na teknolojia katika ngazi ya kata
•Kutoa ushauri kuhusu miradi ya ujenzi, ufundi na teknolojia
•Kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya ujenzi, ufundi na teknolojia
•Kuandaa taarifa ya mwezi, robo mwaka, nusu mwaka na mwaka mzima kuhusu
shughuli zote za ujenzi, ufundi na teknolojia.
8.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye mojawapo ya sifa zilizotajwa hapa chini:
•Waliohitimu kidato cha VI na kufuzu mafunzo ya ufundi ya miaka miwili kutoka Chuo
kinachotambuliwa na Serikali katika fani ya fundi sanifu maendeleo ya jamii
5
•
•
•
Waliohitimu kidato cha IV na kufuzu kozi ya ufundi sanifu maendeleo ya jamii ya
miaka mitatu kutoka Vyuo vya Ufundi vinavyotambuliwa na Serikali katika fani ya
fundi sanifu maendeleo ya jamii
Wenye Cheti cha Majaribio ya Ufundi hatua ya I kutoka Chuo cha Ufundi
kinachotambuliwa na Serikali,
Wenye Stashahada ya Kawaida katika fani za ufundi sanifu maendeleo ya jamii
kutika Chuo kinachotambuliwa na Serikali.
8.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi
9.0 FUNDI SANIFU MSAIDIZI (UMEME) – (ASSISTANT TECHNICIAN - ELECTRICAL) -
NAFASI 17
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na
Halmashauri ya Manispaa ya Temeke
9.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kufanya marekebisho madogo madogo ya umeme katika ofisi na nyumba za serikali.
•Kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.
9.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa waliomaliza kidato cha VI katika masomo ya Sayansi na kufuzu mafunzo ya
mwaka mmoja katika ya fani za Ufundi Umeme kutoka Chuo kinachotambuliwa na
Serikali. AU
•Kuajiriwa waliomaliza kidato cha IV wenye Cheti cha Majaribio ya Ufundi Hatua ya II
kutoka chuocha ufundi katika mojawapo ya fani za ufundi umeme.
9.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.
10.0 FUNDI SANIFU MSAIDIZI (MAJI) (ASISTANT TECHNICIAN - WATER) NAFASI 1
Nafasi hii ni kwa ajili ya Halmashauri ya Mji Njombe
10.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kupima uwingi wa maji mtoni
•Kusoma kituo cha hali ya hewa
•Kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.
10.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha VI waliohudhuria na kufaulu mafunzo ya mwaka
mmoja kutoka kutoka Chuo cha Maji au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali
ambao wana cheti cha ufundi Daraja la III katika fani ya maji.
6
10.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS A kwa mwezi.
11.0 MKUFUNZI DARAJA II (TUTOR GRADE II) – NAFASI 4
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
(Chuo Cha Ardhi Tabora)
NAFASI 2 - Usimamizi na Uthamini wa Ardhi (Land Management and Valuation)
NAFASI 1 - Mipangomiji (Town Planing)
NAFASI 1 - Teknolojia ya Uchapaji (Printing Technology)
11.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kufundisha
•Kutoa ushauri kwa wanachuo katika kazi maalum (projects).
•Kusimamia na kuongoza wanachuo katika kazi za darasani na nje.
•Kutoa ushauri wa kiufundi na kitaalam.
•Kuendesha tafiti na ushauri.
•Kuandaa taarifa za tathmini na mapendekezo ya mitaala ya masomo.
11.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa mwenye Shahada/Stashahada ya Juu katika mojawapo ya fani za
Mipangomiji (Town Planing), Usimamizi na Uthamini wa Ardhi (Land Management
and Valuation), Teknolojia ya Uchapaji (Printing Technology) au Sayansi ya
Kompyuta (Computer Science) kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi au Vyuo Vikuu vingine
vinavyotambuliwa na Serikali.
11.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.E kwa mwezi
12.0 MSANIFU MAJENGO DARAJA LA II (ARCHITECT GRADE II) – NAFASI 7
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Katibu Mkuu
Wizara ya Ujenzi, Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Halmashauri ya Manispaa ya Singida,
Songea na Sumbawanga
12.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kufanya kazi chini ya uangalizi wa Msanifu Majengo aliyesajiliwa na Bodi ya usajili
husika kama “Profession Architect” ili kupata uzoefu unaotakiwa.
•Kufanya kazi kwa vitendo katka fani zinazomhusu ili kumwezesha kupata sifa za
kutosha kusajiliwa na Bodi ya Usajili inayowahusu Wasanifu Majengo
•Kufuatilia upatikanaji wa taarifa na taaluma za za Usanifu wa Majengo
•Kupitia mapendekezo ya miradi (project proposals) mbalimbali ya majengo
7
12.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa wenye Shahada/Stastahada ya Juu ya Uhandisi Sanifu Majengo
(Architects) kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali
12.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali TGS E kwa mwezi.
13.0 FUNDI SANIFU DARAJA II – UCHAPAJI RAMANI (TECHNICIAN GRADE II -
(PHOTOLITHOGRAPHY) – NAFASI 1
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Ajira, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi
13.1 MAJUKUMU YA KAZI
•Kuandaa vifaa vya uchapaji wa ramani, vitabu, vipeperushi
•Kutoa nakala za picha za anga katika uwiano mbalimbali
•Kufanya maandalizi yanayohusu upigaji picha wa ramani na picha za anga
•Kuchapa ramani
13.2 SIFA ZA MWOMBAJI
•Kuajiriwa wenye wahitimu wa kidato cha nne au sita wenye cheti cha mafunzo ua
ufundi ya miaka miwili katika fani ya Uchapaji Ramani (Photolithography)
13.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi
NB: MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.
i.
ii.
iii.
Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania.
Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia
katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi
kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
Nafasi ya kazi inayoombwa iandikwe juu ya bahasha, kutozingatiwa hili kutasababisha
maombi ya kazi kuwa batili.
Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani
na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa
kuaminika.
Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya kidato
cha nne na kidato cha sita kwawale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu
mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Viambatanisho hivyo vibanwe
sawa sawa kuondoa uwezekano wa kudondoka kupotea.
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
- Computer Certificate
8
iv.
v.
vi.
vii.
viii.
ix.
x.
xi.
xii.
xiii.
xiv.
- Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
- Picha moja “Passport size” ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato
cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
Waombaji wawe na umri usiozidi miaka 45.
Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa
kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika
utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika
Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za
kisheria.
Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 10 Agosti, 2012
Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya ajira
HAURUHUSIWI.
Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza na yatumwe kupitia
posta kwa anuani ifuatayo.
Katibu,
Sekretariati ya Ajira katika
Utumishi wa Umma,
SLP.63100,
Dar es Salaam.
AU
Secretary,
Public Service Recruitment
Secretariat,
P.O.Box 63100
Dar es Salaam.
NAFASI ZA KAZI WAKALA WA VIPIMO AUGUSTI 2012
Reviewed by Unknown
on
4:40:00 AM
Rating:
No comments: